VIONGOZI WA KIDINI WATAKIWA KUSHIRIKIANA
Viongozi wa makanisa hapa nchini wametakiwa kuwa na umoja ili kujenga umoja wa makanisa utakaomfanya Kristo ahubiriwe kila mahali kwa ukombozi wa watu wote .
Hayo yamesemwa na Askofu John Mwakyusa wa Kanisa la FPTC, Jimbo la Tanga hivi karibuni katika mahubiri yake.
Askofu Mwakyusa amesema kuwa umoja wa makanisa katika kuinjilisha ndiyo msingi kwa neno la Mungu na kuwa siku zote kama hakuna umoja hakuna Kanisa. Amebainisha kuwa waamini wakikaa kwa umoja hata nchi ni rahisi kukaa kwa umoja kwa sababu misingi yake ipo mioyoni mwa watu wake.
No comments: