MASOMO YA MISA DISEMBA 7, 2017 ALHAMISI JUMA LA 1 LA MAJILIO KUMBUKUMBU YA MT. AMBROSI

SOMO 1:Isa. 26:1-6

Siku ile wimbo huu utaimbwa katika nchi ya Yuda; Sisi tunao mji ulio na nguvu; ataamuru wokovu kuwa kuta na mamboma. Wekeni wazi malango yake, taifa lenye haki, lishikalo kweli, uingie. Utamlinda yeye ambaye moyo wake umekutegemea katika Amani kamilifu, kwa kuwa tunakutumaini.
Mtumainini Bwana sikuzote, maana Bwana Yehova ni mwamba wa milele. Kwa kuwa amewashusha wakaao juu, mji ule ulioinuka, aushusha, aushusha hata nchi, auleta hata mavumbini. Mungu utaukanyaga chini, naam, miguu yao walio maskini, na hatua zao walio wahitaji.



WIMBO WA KATIKATI
Zab. 118:1,8-9,19-21,25-27a (K) 26

(K) Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana.

Mshukuruni Bwana kwa kuwa ni mwema
Kwa maana fadhili zak eni za milele,
Ni heri kumkimbilia Bwana,
Kuliko kuwatumainia wanadamu,
Ni heri kumkimbilia Bwana
Kuliko kuwatumainia wakuu. (K)

Nifungulieni malango ya haki,
Nitaingia na kumshukuru Bwana.
Lango hili ni la Bwana,
Wenye haki ndio watakaoliingia.
Nitakushukuru kwa maana umenijibu,
Nawe umekuwa wokovu wangu. (K)

Ee Bwana, utuokoe, twakusihi,
Na abarikiwe yeye ajaye kwa jina la Bwana,
Tumewabarikia toka nyumbani mwa Bwana.
Bwana ndiye aliye Mungu,
Naye ndiye aliyetupa nuru. (K)

SHANGILIO
Isa. 55:6

Aleluya, aleluya,
Mtafuteni Bwana, maadamu anapatikana, Mwiteni maadamu yu karibu.
Aleluya.

INJILI:Mt. 7:21, 24-27


Siku ili, Yesu akawaambia wafuasi wake: Si kila mtu aniambiaye, Bwana, Bwana, atakayeingia katika ufalme wa mbinguni; bali ni yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye mbinguni.
Basi kila asikiaye hayo maneno yangu, na kuyafanya, atafananishwa na mtu mwenye akili, aliyejenga nyumba yake juu ya mwamba, mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, isianguke; kwa maana misingi yake imewekwa juu ya mwamba.
Na kila asikiaye hayo maneno yangu asiyafanye, atafananishwa na mtu mpumbavu, aliyejenga nyumba juu ya mchanga; mvua ikanyesha, mafuriko yakaja, pepo zikavuma, zikaipiga nyumba ile, ikaanguka; nalo anguko lake likawa kubwa.

No comments:

Powered by Blogger.