MASOMO YA MISA ALHAMISI 3 MEI 2018 SIKUKUU YA WATAKATIFU FILIPO NA YAKOBO

SOMO 1:1Kor.15:1-8


Ndugu zangu, nawaarifu ile injili niliyowahubiri; ambayo ndiyo mliyoipokea, na katika hiyo mnasimama, na kwa hiyo mnaokolewa; ikiwa mnayashika sana maneno niliyowahubiri; isipokuwa mliamini bure.
Kwa maana naliwatolea ninyi hapo mwanzo yale niliyoyapokea mimi mwenyewe, ya kuwa Kristo alikufa kwa ajili ya dhambi zetu, kama yanenavyo maandiko; nay a kuwa alizikwa; nay a kuwa alifufuka siku ya tatu, kama yanenavyo maandiko; nay a kuwa alimtokea Kefa; tena na wale Thenashara; baadaya aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano pamoja; katika hao wengi wanaishi hata Yakobo; tena na mitume wote; na mwisho wa watu wote, alinitokea mimi, kama ni mtu aliyezaliwa si kwa wakati wake.

Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.

WIMBO WA KATIKATI
Zab. 19:1-4 (K) 4

(K) Sauti yao imeenea duniani mwote.

Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu,
Na anga laitangaza kazi ya mikono yake.
Mchana husemezana na mchana,
Usiku hutolea usiku maarifa. (K)

Hakuna lugha wala maneno,
Sauti yao haisikilikani.
Sauti yao imeenea duniani mwote,
Na maneno yao hata miisho ya ulimwengu.
Katika hizo ameliwekea jua hema. (K)

SHANGILIO
Yn. 14:6, 9

Aleluya, aleluya,
Mimi ndimi njia, na kweli na uzima, asema Bwana, Filipo, aliyeniona mimi, amemwona Baba.
Aleluya.

INJILI:Yn.14:8-14


Yesu alimwambia Tomasi: Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Kama mngalinijua, tena mmemwona.
Filipo akamwambia, Bwana, utuonyeshe Baba, yatutosha. Yesu akamwambia, Mimi nimekuwapo pamoja nanyi siku hizi zote, wewe usinijue, Filipo? Aliyeniona mimi amemwona Baba; basi wewe wasemaje, utuonyeshe Baba? Husadiki ya kwamba mimi ni ndani ya Baba, na Baba yu ndani yangu? Hayo maneno niwaambiayo mimi siyasemi kwa shauri langu; lakini Baba, na Baba yu ndani yangu; la! Hamsadiki hivyo, sadikini kwa sababu ya kazi zenyewe.
Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. Nanyi mkiomba lolote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lolote kwa jina langu, nitalifanya.

Neno la Bwana… Sifa kwako Ee Kristu.

No comments:

Powered by Blogger.